Al Ghurair imeshachapisha 90% ya karatasi za kura ya marudio
Published on: October 18, 2017 08:21 (EAT)
Awamu ya kwanza ya karatasi za kupigia kura katika kinyanganyiro cha urais cha wiki ijayo inatarajiwa kuwasili nchini siku ya Jumamosi kutoka Dubai. Kampuni ya Al Ghurair imechapisha zaidi ya asilimia tisini ya karatasi hizo huku Wagombeaji Raila Odinga na Cyrus Jirongo wakijumuishwa licha ya Odinga kujiondoa na Jirongo kufungiwa nje kutokana na kesi dhidi yake ya kufilisika.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment