“Askofu” Deya ashtakiwa hatia ya kuiba watoto
Published on: August 04, 2017 08:26 (EAT)
Baada ya kukwepa mashtaka kwa zaidi ya mwongo mmoja, akiwa nchini Uingereza Askofu Gilbert Deya hatimaye amerejeshwa humu nchini kukabiliana na mashtaka ya jinai.
Askafu huyo anakabiliwa na mashtaka matano ya wizi wa watoto yanayoaminika kutekelezwa humu nchini kati ya mwaka wa 1999 na 2004. Deya alirejeshwa humu nchini mapema hii leo, na kusafirishwa moja kwa moja hadi kwenye makao makuu ya CID kabla ya kufikishwa mahakamani muda mfupi baadaye.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment