Binti wa mbunge ni “gaidi”?
Mahakama imemuagiza mbunge wa eneo la Mugirango Kaskazini Charles Mong’are kufika mbele yake hapo Jumatatu ili kuelezea anachokijua kuhusiana na madai ya ugaidi yanayomwandama mwanawe msichana anayefahamika kama Erishna Mong’are. Erishna na mpenziwe kwa jina Ahmed Lali walikamatwa hapo jana humu jijini na kufikishwa mahakamani hii leo waliposhtakiwa na madai ya kuhusika katika kupanga visa vya ugaidi huku ikidaiwa kwamba wawili hao walikuwa na nia ya kutorokea taifa jirani la Tanzania kabla ya mwisho wa mwezi huu.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment