Chama cha ODM kimewafurusha wanachama 10 waasi
Chama cha ODM kimewafurusha wanachama 10 waasi, akiwemo gavana wa kwale Salim Mvurya na wabunge saba. baraza kuu la ODM, katika uamuzi wa pamoja, limemtaka msajili wa vyama vya kisiasa bi lucy ndung’u kuwaondoa kwenye sajili rasmi ya chama, wabunge Ababu Namwamba, Isaac Mwaura, John Waluke, Zainab Chidzuga na Masuoud Mwahima. hata hivyo gavana wa marsabit Ukur Yatani na mbunge wa igembe ya kati Iringo Kubai wamepewa msamaha huku wabunge wawili waasi wa kaunti ya kisii Richard Onyonka na Simeon Ogari wakikabaliwa na wakati mgumu, licha ya kuamua kurejea chamani na kuomba msamaha.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment