Clinton anaongoza kwenye kura ya maoni dhidi ya Trump
Huku Zikiwa zimesalia wiki mbili tu kabla ya uchaguzi wa Marekani kufanyika, wagombea wa urais, Donald Trump na Hillary Clinton, wameongeza kasi kwenye kampeni zao, na kuanza kufanya mikutano mingi ya kuwarai wapiga kura, kuliko ilivyokuwa hapo awali, hususan kwenye majimbo ambayo yana ushindani mkubwa kisiasa.
Siku ya Alhamisi, Trump wa chama cha Republican na Clinton wa chama cha Democratic, walikutana mjini New York, kwenye hafla ya chakula cha jioni, ambako walitoa hotuba zilizojaa kejeli na vichekesho.
Lakini maswala yaliyoibuka kwenye mdahalo ulifaonyika siku ya Jumatano, ndiyo yanayoendelea kuzua gumzo Zaidi, kati ya Wamerekani wengi.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment