Duale aandikisha taarifa kuhusu matamshi ya chuki
Published on: January 06, 2017 08:36 (EAT)
Kiongozi wa wengi bungeni Aden Duale anaandikisha taarifa katika makao makuu ya upelelezi wa jinai kuhusu matamshi yanayokisiwa kuwa ya uchochezi wa kikabila. Duale alinukuliwa akiwaelekeza jamii ya Wakamba wasipeleke siasa za Wiper katika kaunti ya Garissa. Viongozi mbalimbali wamemkashifu Duale kuhusiana na matamshi hayo huku mwenyekiti wa tume ya maridhiano Francis Ole Kaparo akitaka uchunguzi kuhusiana na madai hayo kufanyika.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment