EACC yamhoji Muraguri kuhusiana na ubadhirifu wa fedha
Katibu katika wizara ya afya Nicholus Muraguri adhuhuri ya leo alihojiwa na maafisa wa tume ya kupambana na ufisadi (EACC), kujibu maswali kuambatana na madai ya kupotea kwa mabilioni ya pesa katika wizara yake.
Duru za kuaminika ziliarifu Citizen nipashe kuwa mahojiano hayo yaliyochukua zaidi ya saa tatu yaliegemea ubadhirifu wa fedha na uhusiano wake na maafisa wengine katika wizara hiyo.
Na kama anavyoarifu Hassan Mugambi haya yanajiri huku mashirika ya kujamii yakipanga maandamano dhidi ya muraguri na waziri wa afya Cleopa Mailu.
Want to send us a story? Submit on Wananchi Reporting on the Citizen Digital App or Send an email to wananchi@royalmedia.co.ke or Send an SMS to 25170 or WhatsApp on 0743570000
Comments
No comments yet.
Leave a Comment