George Okode achaguliwa tena kuwa spika wa bunge la Siaya

Bunge la kaunti ya Siaya limeanza rasmi vikao vyake leo ambapo wawakilishi wa wadi wameapishwa na kisha kumchagua spika
Kiapo cha madiwani wapya kimeongozwa na makarani wa bunge hilo. Spika wa bunge lililopita George Okode amefanikiwa kuhifadhi kiti chake baada ya kuwashinda wapinzani wake kwa kura nyingi. Okode amepata kura 33 huku mpinzani wake wa karibu George Rubik, akipata kura 8. Wengine waliotafuta kiti hicho ni pamoja na Nicholas Abidha na Samuel Muga ambao hawakupata hata kura moja.

Tags:

SIAYA COUNTY George Okode

Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke

Leave a Comment

Comments

No comments yet.

latest stories