Hatua ya Bahati kukalia kiti cha rais yaibua hisia mseto
Kuzinduliwa rasmi kwa chama cha Jubilee hapo jana kuliambatana na mbwembwe na madoido ya aina yake lakini kile ambacho kimesalia vinywani mwa wakenya wengi ni tumbuizo la mwanamuziki wa nyimbo za injili Kevin Bahati almaarufu ‘Bahati’. Hatua yake ya kumwondoa Rais Uhuru Kenyatta kwenye kiti chake na kukalia kisha kumwimbia mama wa taifa Margaret Kenyatta pamoja na kuweka mguu wake juu ya meza ya naibu rais William Ruto imezua hisia mseto huku wengi wakilalamika kuwa alivuka mipaka.
Want to send us a story? Submit on Wananchi Reporting on the Citizen Digital App or Send an email to wananchi@royalmedia.co.ke or Send an SMS to 25170 or WhatsApp on 0743570000
Comments
No comments yet.
Leave a Comment