Hisia mseto zatolewa kuhusu mauaji ya majambazi wanne na polisi Eastleigh
Published on: April 01, 2017 08:27 (EAT)
Washukiwa wanane wa ujambazi waliuawa jana huku afisa mmoja wa polisi akipoteza maisha yake katika mojawapo wa matukio ya kutamausha mtaani Eastleigh hapa jijini Nairobi. Katika video moja ambayo imezua tetesi kali inaonesha kijana mmoja akipigwa risasi hadharani na mtu anayeaminika kuwa afisa wa polisi. Ni video ambayo inaendelea kujadiliwa huku baadhi wakighadhabishwa na jinsi polisi anavyotumia nguvu na wengine wakiunga mkono mauaji hayo wakisema wanazidi kuhangaishwa na majambazi sugu mtaani humo.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment