Huenda orodha ya mawaziri wapya ikawasilishwa bungeni Jumanne

Huenda baraza la mawaziri litakatangazwa kabla ya krismasi. Inaarifiwa kuwa Rais Uhuru Kenyatta na naibu Rais William Ruto tayari wameshaafikia majina ya watakaoteuliwa kuhudumu katika baraza hilo. Duru zaarifu kuwa majina hayo yatawasilishwa bungeni Jumanne baada ya mkutano wa hapo kesho kati ya Rais Kenyatta, maspika wa bunge na viongozi wa wengi bungeni. Inaarifiwa kuwa bunge litakamilisha uchunguzi wa wateule kufikia tarehe ishirini mwezi huu.

Tags:

President Uhuru Kenyatta Cabinet

Want to send us a story? Submit on Wananchi Reporting on the Citizen Digital App or Send an email to wananchi@royalmedia.co.ke or Send an SMS to 25170 or WhatsApp on 0743570000

Leave a Comment

Comments

No comments yet.

latest stories