Huenda siku ya uchaguzi wa urais ikabadilishwa

Uchaguzi mpya wa urais huenda usiandaliwe tarehe 17 mwezi ujao kama ilivyotangazwa na tume ya uchaguzi nchini-IEBC. Ingawa sababu kadhaa za mabadiliko ya tarehe hiyo zinatolewa na wadau, tarehe mpya ya uchaguzi itaathiri kalenda ya mitihani ya kitaifa ya darasa la nane na kidato cha nne inayotarajiwa kung’oa nanga mwezi ujao. Ingawa IEBC haijatangaza tarehe mpya ya uchaguzi wa urais, imewaalika Rais Uhuru Kenyatta na kinara wa Nasa Raila Odinga au waakilishi wao katika mkutano siku ya Jumatano, kushauriana kuhusu masuala nyeti na maandalizi ya mchuano mpya wa ikulu.

Tags:

IEBC JUBILEE NASA election date

Want to send us a story? Submit on Wananchi Reporting on the Citizen Digital App or Send an email to wananchi@royalmedia.co.ke or Send an SMS to 25170 or WhatsApp on 0743570000

Leave a Comment

Comments

No comments yet.

latest stories