Huenda uchaguzi ukaahirishwa maeneo kadhaa
Published on: October 21, 2017 08:05 (EAT)
Tume ya uchaguzi nchini IEBC inapendekeza kuahirisha uchaguzi wa urais katika maeneo yatakayokumbwa na suitafahamu siku ya Alhamisi. Pendekezo hilo lilijadiliwa na kamati maalum iliyobuniwa na mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati katika kikao kilichoandaliwa hapo jana katika ukumbi wa Bomas. IEBC inapendekeza kutumia kipengee 73 cha sheria za uchaguzi, kuahirisha mchuano wa urais haswa katika maeneo yanayomshabikia sana kinara wa nasa raila odinga.
Want to send us a story? Submit on Wananchi Reporting on the Citizen Digital App or Send an email to wananchi@royalmedia.co.ke or Send an SMS to 25170 or WhatsApp on 0743570000
Comments
No comments yet.
Leave a Comment