Huenda uchaguzi ukaahirishwa maeneo kadhaa
Published on: October 21, 2017 08:05 (EAT)
Tume ya uchaguzi nchini IEBC inapendekeza kuahirisha uchaguzi wa urais katika maeneo yatakayokumbwa na suitafahamu siku ya Alhamisi. Pendekezo hilo lilijadiliwa na kamati maalum iliyobuniwa na mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati katika kikao kilichoandaliwa hapo jana katika ukumbi wa Bomas. IEBC inapendekeza kutumia kipengee 73 cha sheria za uchaguzi, kuahirisha mchuano wa urais haswa katika maeneo yanayomshabikia sana kinara wa nasa raila odinga.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment