IEBC yabadilisha tarehe ya uchaguzi kutoka Okt 17
Published on: September 21, 2017 08:59 (EAT)
Uchaguzi wa urais utafanyika tarehe ishirini na sita mwezi ujao. Tarehe hiyo imeafikiwa na tume ya uchaguzi nchini baada ya kuchunguza hukumu ya kina iliyotolewa na mahakama ya upeo hapo jana. IEBC inasema kuwa imelazimika kuahirisha uchaguzi ili kuweza kuweka sawa kimikakati yote iliyoratibiwa na mahakama ya upeo ili uchaguzi uwe huru na wa haki.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment