IEBC yakagua maandalizi ya uchaguzi katika kanda ya Nyanza
Baadhi ya maafisa wa tume ya IEBC katika eneo la Nyanza wameelezea hofu katika kuandaa marudio ya uchaguzi wa urais wakisema hali ya usalama ni ya kutatanisha. Maafisa hao ambao waliweka wazi hisia zao kwa kamishana wa IEBC Roselyn Akombe wanaitaka tume kutafuta suluhu ikizingatiwa Kinara wa NASA Raila Odinga amejiondoa kwenye kinyang’anyiro huku maeneo hayo yakishuhudia visa vya utovu wa usalama na maandamano dhidi ya IEBC. haya yanajiri huku Mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati akishikilia uchaguzi utaendelea na kamwe hatang’atuka.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment