IEBC yakutana na viongozi wa kidini
Published on: March 01, 2017 08:29 (EAT)
Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi na mipaka nchini wafula chebukati ametoa hakikisho kwa wakenya kuwa tume hiyo iko tayari kuandaa uchaguzi wa agosti mwaka huu, kinyume na madai ya baadhi ya wanasiasa. Akizungumza huko limuru katika hafla iliyoandaliwa na baraza la makanisa nchini ncck, chebukati alisema bado wana muda wa kununua mfumo wa kiteknolojia wa kuandaa uchaguzi huku wakinuia kufanya hivyo kabla ya mwisho wa mwezi huu.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment