Jaji mkuu David Maraga ahimiza ushirikiano serikalini
Published on: December 15, 2017 07:51 (EAT)
Jaji Mkuu David Maraga ameyataka matawi matatu ya serikali kushirikiana katika kuwahudumia wakenya na kutojihusisha na mikwaruzano akisema Bunge, Idara ya Mahakama na serikali kuu zinafaa kuheshimu uhuru wa kila moja. Maraga amesema haya alipozindua ripoti ya idara ya mahakama ya mwaka wa 2016/2017, hafla iliyohudhuriwa na Rais Uhuru Kenyatta ambaye amemtaka Jaji Mkuu kushauriana na matawi mengine katika kutatua masuala yanayoibuka hasa yanayohusu umma.
Want to send us a story? Submit on Wananchi Reporting on the Citizen Digital App or Send an email to wananchi@royalmedia.co.ke or Send an SMS to 25170 or WhatsApp on 0743570000
Comments
No comments yet.
Leave a Comment