Jamaa asalimisha bastola kwa maafisa wa polisi
Published on: October 08, 2016 10:34 (EAT)
Mwanamme mwenye umri wa miaka 21 amesalimisha bastola ndogo kwa maafisa wa polisi kaitka eneo bunge la Starehe, baada ya miaka sita ya kushiriki kwenye visa vya uhalifu. Kijana huyo ambaye anasema alishawishiwa na mhubiri wa kanisa la Faith Evangelistic huko Korogocho kuchukua hatua hiyo hata hivyo amepata msamaha wa polisi, ijapokuwa msimamizi wa polisi Nairobi Japheth Koome anasema endapo mlalamishi yeyote atajitokeza, basi uchunguzi unaweza kuanzishwa.
Want to send us a story? Submit on Wananchi Reporting on the Citizen Digital App or Send an email to wananchi@royalmedia.co.ke or Send an SMS to 25170 or WhatsApp on 0743570000
Comments
No comments yet.
Leave a Comment