Jubilee waingia Nairobi
Rais Uhuru Kenyatta amewahakikishia wenyeji wa Nairobi na taifa kwa jumla usalama wao, huku uchaguzi mkuu ukizidi kubisha hodi. Kenyatta amesema hakuna haja ya Mkenya yeyote kutoroka anapoishi au kufanyia biashara, akihofia ghasia kuzuka na kuagiza vitengo vya usalama kukabiliana na wale wanaochochea uhasama. Jubilee imetetea utendakazi wake miaka minne uongozini, na kuwarai Wakenya kuidhinisha kibwagizo cha Uhuru-Ruto Tano Tena, huku wakiwasuta wapinzani wao kama wasio na dira ya kulielekeza kimaendeleo.
Want to send us a story? Submit on Wananchi Reporting on the Citizen Digital App or Send an email to wananchi@royalmedia.co.ke or Send an SMS to 25170 or WhatsApp on 0743570000
Comments
No comments yet.
Leave a Comment