Jubilee wakataa maafisa waliotajwa na Chebukati
Mirengo ya Jubilee na Nasa inazidi kuzozana kuhusu maandalizi ya uchaguzi mpya wa urais, kama ilivyoagizwa na mahakama ya juu nchini. Jubilee imepinga mabadiliko ya uongozi katika secretariat ya IEBC, na kudai Marjan Hussein aliyeteuliwa kuongoza shughuli za kinyang’anyiro kipya cha ikulu ni mshirika wa karibu wa Nasa. Kwa upande wake, Nasa inashinikiza kuondolewa kabisa kwa afisa mkuu mtendaji wa IEBC Ezra Chiloba na wakurugenzi sita wa IEBC, na pia kuhusishwa katika upekuzi wa mitambo ili kufanikisha uchaguzi huru na haki.
Want to send us a story? Submit on Wananchi Reporting on the Citizen Digital App or Send an email to wananchi@royalmedia.co.ke or Send an SMS to 25170 or WhatsApp on 0743570000
Comments
No comments yet.
Leave a Comment