Kamama amulikwa

Mbunge wa Tiaty Asman Kamama ataondolewa kutoka wadhifa wa mwenyekiti wa kamati ya usalama katika bunge la kitaifa juma lijalo, kutokana na dhana ya kutumia wadhifa wake kuhujumu shughuli za kuwafurusha wahalifu wa wizi wa mifugo kaunti ya Baringo. Licha ya Kamama kusisitiza hana hatia, kiongozi wa wengi katika bunge la kitaifa Aden Duale amedokeza kuwa Kamama atahamishiwa katika kamati nyingine, huku ikiarifiwa kuwa mbunge wa Kigumo Jamleck Kamau huenda akaurithi wadhifa huo.

Tags:

baringo Tiaty Jamleck Kamau Asman Kamama Kamati ya usalama

Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke

Leave a Comment

Comments

No comments yet.

latest stories