Kamati ya bunge yamhoji dereva anayehusishwa na sakata ya NYS
Published on: October 27, 2016 09:22 (EAT)
Kamati ya bunge inayochunguza sakata ya NYS hii leo ilimhoji John Kago aliyehudumu kama dereva katika benki ya KCB ambaye sasa ni milionea. John kago yadaiwa kuwa shilingi milioni mia tatu arobaini na sita kutoka kikapu cha NYS yaliingia kwenye akaunti zake mbili, huku washukiwa wakuu Ben Gethi na Josphine Kabura wakimpa zaidi ya shilingi milioni mia moja kila mmoja. Dereva huyo aliyegeuka milionea hata hivyo alikana kupokea mamilioni ya pesa kutoka idara ya NYS.
Want to send us a story? Submit on Wananchi Reporting on the Citizen Digital App or Send an email to wananchi@royalmedia.co.ke or Send an SMS to 25170 or WhatsApp on 0743570000
Comments
No comments yet.
Leave a Comment