Kamati ya sheria yapendekeza Kinisu atimuliwe

Kamati ya sheria katika bunge la kitaifa imependekeza mwenyekiti wa tume ya maadili na kukabiliana na ufisadi Phillip Kinisu atimuliwe, kwa kukosa maadili na kuwa na uhusiano wa kibinafsi na kampuni iliyokuwa ikichunguzwa na tume hiyo. Kamati ya Jlac, kwa wingi wa kura, inalitaka bunge kupendekeza Rais Uhuru Kenyatta abuni jopo la kumchunguza kinisu, kwa madai kuwa hakudokeza ana uhusiano na kampuni ya Esaki Limited, iliyokuwa ikichunguzwa kwa kuhusika katika sakata ya huduma kwa vijana(Nys). Francis Gachuri ana taarifa kamili.

Want to send us a story? Submit on Wananchi Reporting on the Citizen Digital App or Send an email to wananchi@royalmedia.co.ke or Send an SMS to 25170 or WhatsApp on 0743570000

Leave a Comment

Comments

No comments yet.

latest stories