Kashfa ya afya
Maandamano yaliyokuwa yamepangwa na baadhi ya mashirika ya kijamii jijini nairobi kulalamikia kukithiri kwa ufisadi serikalini yalitibuliwa na maafisa wa polisi waliowarushia waandamanaji vitoa machozi.
Katika kile kilichoonekana kama kuziba ukweli wa mambo maafisa hao waliwageukia wanahabari na kuwafurusha kwa vitoamachozi huku mpigapicha wa shirika la west media akijipata pabaya.
Haya yanajiri huku waziri wa afya cleopha mailu aliyehojiwa na maafisa wa tume ya kupambana na ufisadi hii leo akishikilia msimamo wake na kusema kamwe hatojiuzulu.
Want to send us a story? Submit on Wananchi Reporting on the Citizen Digital App or Send an email to wananchi@royalmedia.co.ke or Send an SMS to 25170 or WhatsApp on 0743570000
Comments
No comments yet.
Leave a Comment