Kenya itawaajiri madaktari 500 kutoka Tanzania
Published on: March 18, 2017 09:08 (EAT)
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeidhinisha kuajiriwa kwa madaktari 500 katika hospitali za humu nchini. Hii ni kufuatia ombi la Rais Kenyatta kwa serikali hiyo.
Rais John Pombe Magufuli amesema kuwa madaktari wanaoruhusiwa ni wale ambao hawana kazi. Hata hivyo chama cha madaktari nchini- KMPDU- kinateta na kuitaka serikali kuwaajiri kwanza madaktari 1400 wa humu nchini, ambao hawajaajiriwa.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment