Kesi ya Mauaji ya Monica Kimani: Maribe, Jowie kusalia rumande

Kesi ya Mauaji ya Monica Kimani: Maribe, Jowie kusalia rumande

Mwanahabari wa runinga Citizen Jacque Maribe pamoja na Joseph Irungu ambaye ni mshukiwa mkuu wa mauaji ya Monica Kimani wamefikishwa mahakamani na kukanusha mashtaka ya mauaji ya binti huyo.

Jaji Jessie Lessit aliamuru wawili hao kusalia rumande hadi siku ya Jumatano wakati ambapo ombi la kutaka kuachiliwa kwao kwa dhamana litasikilizwa.

Hata hivyo upande wa mashtaka umetoa sababu kadhaa za kukataa wawili hao kuachiliwa kwa dhamana.

Mawakili wa serikali wamesema kuwa wawili hao hawapasi kuachiliwa kwa kuwa huenda wakatatiza uchunguzi.

Kwa mujibu wa stakabadhi zilizowasilishwa mahakamani, ukosefu wa makao rasmi ya Joseph Irungu na ushawishi wa Maribe kutokana na kazi yake ya uanahabari huenda zikaingilia uchunguzi.

Na sasa swala nzima la dhamana litapelekwa mbele ya jaji mwingine wa mahakama kuu na kusikizwa siku ya Jumatano.

Wawili hao watasalia rumande hadi siku hiyo ambapo ombi lao la kuachiliwa kwa dhamana litaangaziwa.

Tags:

Jacque Maribe monica kimani

Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke

Leave a Comment

Comments

No comments yet.

latest stories