Kifaru Mweupe Asalia Pekee Ulimwenguni
Published on: April 20, 2015 06:35 (EAT)
Ni mnyama ambaye ameendelea kugonga vichwa vya habari sio tu hapa nchini bali kote ulimwenguni kutokana na hofu ya kuadimika kwa kizazi chake. Katika ulimwengu mzima ni kifaru dume mmoja mweupe aliyesalia na ambaye hawezi kuzalisha kufuatia umri wake. Wa kike wamesalia wanne tu. Pheona Kengah alizuru mbuga la wanyama la Ol Pejeta na kutuandalia taarifa kuhusu kifaru huyo kwa jina Sudan aliye chini ya ulinzi mkali masaa 24 kutokana na wawindaji haramu.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment