Kikosi cha NASA chaomba kura Tharaka Nithi
Published on: June 16, 2017 08:01 (EAT)
Viongozi wa muungano wa NASA walikita kambi katika kaunti ya Tharaka Nithi ambapo waliwarai wananchi kuwabwaga Rais Uhuru Kenyatta na naibu wake William Ruto na badala yake kuwaunga wao mkono. Wakiongozwa na mgombea urais Raila Odinga, viongozi hao walisema kuwa Jubilee imewahadaa wananchi kwa miaka minne na hakuna maendeleo yoyote ambayo wamewafanyia wana Tharaka Nithi.
Want to send us a story? Submit on Wananchi Reporting on the Citizen Digital App or Send an email to wananchi@royalmedia.co.ke or Send an SMS to 25170 or WhatsApp on 0743570000
Comments
No comments yet.
Leave a Comment