Kizungumkuti cha mahindi: Waziri Kiunjuri ahojiwa na Seneti
Published on: October 25, 2018 03:35 (EAT)
Waziri wa Kilimo Mwangi Kiunjuri leo amehojiwa na kamati maalum ya bunge la seneti inayochunguza utata wa malipo ya mahindi nchini.
Kiunjuri ametakiwa kueleza utata unaogubika malipo hayo ambapo amewaambia maseneta kuwa serikali tayari imelipa shilingi bilioni 9.4 kwa zaidi ya tani milioni tatu za mahindi wakati wa msimu wa mwaka wa 2017/2018.
Waziri pia ametakiwa kutoa hakikisho kuwa Kenya kuna usalama wa chakula.
Want to send us a story? Submit on Wananchi Reporting on the Citizen Digital App or Send an email to wananchi@royalmedia.co.ke or Send an SMS to 25170 or WhatsApp on 0743570000
Comments
No comments yet.
Leave a Comment