Korti yasitisha pendekezo la kupunguza mishahara ya wabunge
Mahakama kuu imesitisha kwa muda, utekelezaji wa utaratibu wa kupunguza mishahara na marupurupu ya wabunge ulioasisiwa na tume ya mishahara nchini (SRC). Jaji George Odunga alitoa agizo hilo baada ya tume ya huduma za bunge (PSC) kuwasilisha kesi, na kudai SRC iliwadhulumu wabunge na haikuzingatia gharama yao ya maisha ilipopiga wembe mishahara yao. Kando na kupokea mshahara wa takriban shilingi milioni moja kila mmoja, wabunge sasa wataweza kupokea marupurupu ya usafiri, magari na mikopo ya nyumba.
Want to send us a story? Submit on Wananchi Reporting on the Citizen Digital App or Send an email to wananchi@royalmedia.co.ke or Send an SMS to 25170 or WhatsApp on 0743570000
Comments
No comments yet.
Leave a Comment