Maafisa wa IEBC wazuiwa kutoa mafunzo huko Bondo
Huenda tume ya uchaguzi ikafutilia mbali uchaguzi wa terehe 26 katika baadhi ya maeneo ambapo usalama wa maafisa wa uchaguzi unatiliwa shaka. Haya ni baada ya maafisa kususia mafunzo na baadhi kutimuliwa na makundi ya watu katika maeneo ya Nyanza na magharibi mwa nchi. Naibu mwenyekiti wa IEBC Consolata Nkatha anasema kuwa tume hiyo itatathmini vitisho dhidi ya maafisa wake kabla ya kutoa mwelekeo. Haya ni huku mahakama ya upeo ikisema kuwa mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati hana mamlaka yoyote ya kubadilisha matokeo ya uchaguzi.
Want to send us a story? Submit on Wananchi Reporting on the Citizen Digital App or Send an email to wananchi@royalmedia.co.ke or Send an SMS to 25170 or WhatsApp on 0743570000
Comments
No comments yet.
Leave a Comment