Magaidi waangamiza watu 4 huko Hindi, Lamu

Watu wanaoshukiwa kuwa wanamgambo wa Al Shabaab wamewaangamiza watu 4 katika eneo la hindi kaunti ya Lamu. Mashambulizi hayo yamefanyika katika vijiji viwili tofauti, kisa cha kwanza kilifanyika katika kijiji cha Bobo mwendo wa saa kumi na mbili na nusu siku ya Jumanne na kingine kufanyika mwendo wa saa saba na nusu usiku wa kuamkia leo katika kijiji cha silini-mashambani.
Wanamgambo hao walikuwa na bunduki aina ya AK 47, na walizunguka vijiji hivyo wakiamuru watu kutoka katika nyumba zao kabla ya kutekeleza mauaji. Kulingana na kamishna wa kaunti ya lamu, gilbert kitiyo hali hii ni ya kutamausha kwani wanamgambo hao walikuwa wakitaja majina ya wahanga wao kabla ya kuwachinja. Haya yanajiri huku operesheni ya kuwasaka magaidi hao ikiendelea.

Tags:

lamu Al Shabaab Panda Nguo Bobo Silini mashambani

Want to send us a story? Submit on Wananchi Reporting on the Citizen Digital App or Send an email to wananchi@royalmedia.co.ke or Send an SMS to 25170 or WhatsApp on 0743570000

Leave a Comment

Comments

No comments yet.

latest stories