Makachero wa EACC wavamia wizara ya afya
Published on: October 28, 2016 09:52 (EAT)
Makachero kutoka tume ya kupambana na ufisadi nchini, EACC hii leo walivamia makao makuu ya wizara ya afya huku uchunguzi dhidi ya kupotea kwa shilingi bilioni tano kukianza. Naibu mwenyekiti wa tume ya EACC, Michael Mubea, amesema kuwa wameunda timu maalum itakayochunguza sakata hiyo. Haya yanajiri huku waziri wa afya Cleopa Mailu akipinga vikali kuwepo kwa ufisadi katika wizara yake.
Want to send us a story? Submit on Wananchi Reporting on the Citizen Digital App or Send an email to wananchi@royalmedia.co.ke or Send an SMS to 25170 or WhatsApp on 0743570000
Comments
No comments yet.
Leave a Comment