Mama ateketea Baringo

Mama ateketea Baringo

Mwanamke mmoja amefariki kutokana na moto unaoaminika kusababishwa na mlipuko wa jiko la stovu uliosambaa na kuchoma nyumba kadhaa usiku wa kuamkia leo eneo la Bondeni, Baringo ya Kati.

Walioshuhudia wanasema mlipuko huo ulisikika mwendo wa saa sita usiku na kufuatiwa na moto mkubwa uliowashinda kuudhibiti.

Wakaazi wametoa wito kwa idara ya kushughulikia majanga ya moto kaunti ya baringo iwe macho kunapotokea ajali za moto.

Mtu mmoja aliyepata majeraha amepelekwa katika hospitali ya rufaa ya kabarnet kwa matibabu zaidi.

Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke

Leave a Comment

Comments

No comments yet.

latest stories