Maraga: Tunaendelea kuandika uamuzi
Published on: November 18, 2017 08:13 (EAT)
Jaji Mkuu David Maraga anasema Majaji sita wa mahakama ya upeo wangali wanaandika uamuzi wao kuhusu kesi mbili zinazonuia kubatilisha uchaguzi wa Oktoba 26 uliompa Uhuru Kenyatta Ushindi. Akizungumza baada ya kuhudhuria ibada ya kanisani hapa Nairobi Maraga anasema watatoa uamuzi huo saa tano siku ya Jumatatu, majaji hao wakiaminika kuwa wanaandika uamuzi wa kila mmoja binafsi kabla ya kukutana kuwianisha misimamo.
Want to send us a story? Submit on Wananchi Reporting on the Citizen Digital App or Send an email to wananchi@royalmedia.co.ke or Send an SMS to 25170 or WhatsApp on 0743570000
Comments
No comments yet.
Leave a Comment