Marehemu Gavana Gakuru kuzikwa tarehe 18
Published on: November 08, 2017 08:16 (EAT)
Marehemu gavana wa Nyeri Gakuru Wahome huenda akazikwa tarehe kumi na nane mwezi huu, akipata mazishi ya kitaifa yatakayofadhiliwa na serikali. Waziri wa mawasiliano ambaye pia ni mwenyekiti mwenza wa kamati ya mazishi anasema uamuzi huo umeafikiwa kuambatana na hadhi ya Wahome huku maandalizi ya mazishi nyumbani kwake huko Nyeri yakianza. Haya yanajiri huku hafla ya kumwapisha naibu gavana wa Nyeri Mutahi Kahiga ambayo ilitarajiwa kufanyika hapo kesho ikiahirishwa.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment