Mawakili wa Uhuru wasema alishinda kwa haki

Rais Uhuru Kenyatta ameutetea ushindi wake katika mchuano wa ikulu ulioandaliwa tarehe nane mwezi huu na kusimamiwa na tume ya uchaguzi nchini-IEBC. Kenyatta kupitia kwa mawakili wake Fred Ngatia, Ahmednassir Abdulahi na Tom Macharia amesema kesi iliyowasilishwa na kinara wa Nasa Raila Odinga haina uzito wowote kisheria, wala ushahidi muafaka kuthibitisha madai ya wizi wa kura na udukuzi wa mitambo ya IEBC. Aidha, Kenyatta amesema kubatilisha ushindi wake ni sawa na kukiuka haki ya wakenya kuwachagua viongozi bila kushurutishwa.

Tags:

Uhuru kenyatta supreme court ahmednassir abdullahi PRESIDENTIAL PETITION Fred Ngatia

Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke

Leave a Comment

Comments

No comments yet.

latest stories