Mbunge wa Nyeri mjini aomba JSC imfute kazi Jaji Maraga
Published on: September 14, 2017 08:59 (EAT)
Mbunge wa Nyeri mjini Wambugu Ngunjiri ameiomba tume inayosimamia idara ya mahakama JSC kumchunguza Jaji Mkuu David Maraga kwa lengo la kumwondoa afisini, akisema alivunja sheria katika uamuzi wa kesi dhidi ya matokeo ya urais ambapo alifutilia mbali kuchaguliwa kwa rais Uhuru Kenyatta. Maombi ya Ngunjiri hata hivyo yamekemewa na viongozi kadhaa kutoka Jubilee na NASA huku wale kutoka eneo la kisii chini ya Jubilee wakimtaka Wambugu kuondoa ombi hilo kufikia kesho.
Want to send us a story? Submit on Wananchi Reporting on the Citizen Digital App or Send an email to wananchi@royalmedia.co.ke or Send an SMS to 25170 or WhatsApp on 0743570000
Comments
No comments yet.
Leave a Comment