Moshi mweupe umefuka kwenye mazungumzo ya IEBC
Published on: August 16, 2016 08:06 (EAT)
Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi nchini-IEBC Ahmed Issack Hassan na makamishna wenzake wanafaa kuondoka ofisini kufikia tarehe 30, mwezi ujao. Kamati teule ya bunge imependekeza makamishna wapya saba wa IEBC wateuliwe na jopo maalum na kuidhinishwa na bunge katika muda wa siku 50, na majukumu yao kuwekwa bayana. Aidha, chuma cha wanasiasa wenye mazoea ya kuhamahama vyama baada ya kufeli wakati wa kura za mchujo ki motoni.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment