Msichana aliyeuawa pamoja na Msando pia alinyongwa
Published on: August 03, 2017 09:04 (EAT)
Upasuaji wa maiti ya Maryanne Ngumbu, msichana wa miaka 21 ambaye mwili wake ulipatikana pamoja na ule wa mkurugenzi wa masuala ya teknolojia katika wa tume ya IEBC Chris Msando, umeonyesha kuwa aliuawa kwa kunyongwa kutumia kamba.
Haya yanajiri huku watu wengine watatu wanaoaminika kuhusika katika mauaji hayo wakitiwa mbaroni na kupelekea idadi ya waliokamatwa kuwa sita kufikia sasa.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment