Muhoro ahojiwa na wabunge kuhusu ufujaji wa hazina ya vijana
Published on: February 09, 2017 08:35 (EAT)
Serikali imesitisha uuzaji wa nyumba iliyogharimu zaidi ya milioni 48 zinazodhaniwa kuibwa kutoka kwa hazina ya vijana yapata miaka miwili iliyopita. Mkurugenzi wa shirika la upelelezi Ndegwa Muhoro ameiambia kamati ya bunge kuwa watu kadhaa wakiwemo maafisa wakuu wa zamani wa hazina ya vijana Bruce Odhiambo na Catherine Namuye wangali wanakabiliwa na kesi mahakamani akisema changamoto za kisheria ndizo zinazochelewesha kukamilika kwa kesi hizo.
Want to send us a story? Submit on Wananchi Reporting on the Citizen Digital App or Send an email to wananchi@royalmedia.co.ke or Send an SMS to 25170 or WhatsApp on 0743570000
Comments
No comments yet.
Leave a Comment