Muungano wa NASA uliwasilisha kesi mahakamani jana

Kinara wa NASA Raila Odinga usiku wa jana aliwasilisha kesi katika mahakama ya juu zaidi nchini, kupinga uchaguzi wa Rais Uhuru Kenyatta na Naibu wake kuhudumu kwa muhula wa pili. Odinga, katika ombi lake lenye zaidi ya kurasa 25,000 kwa majaji saba wa mahakama hiyo, anashinikiza matokeo ya mchuano wa urais yabatilishwe na uchaguzi mpya kuandaliwa. Francis Gachuri ana taarifa kamili kuhusu kesi ya NASA.

Want to send us a story? Submit on Wananchi Reporting on the Citizen Digital App or Send an email to wananchi@royalmedia.co.ke or Send an SMS to 25170 or WhatsApp on 0743570000

Leave a Comment

Comments

No comments yet.

latest stories