Mwanafunzi anayedaiwa kuwasha moto shule ya Moi ashtakiwa
Published on: September 06, 2017 08:22 (EAT)
Mahakama ya watoto imeruhusu maafisa wa upelelezi wanaoendeleza uchunguzi wa mkasa wa moto katika shule ya upili ya wasichana ya Moi hapa jijini Nairobi kumzuilia mshukiwa mmoja kwa siku saba wanapoendeleza uchunguzi. Mshukiwa ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha kwanza atazuiliwa katika kituo cha polisi cha Kilimani hadi Jumatano ijayo huku maafisa wakipekuapekua baadhi ya ushahidi walionao zikiwemo simu yake ya rununu na kipakatalishi, zilizochukuliwa nyumbani kwao hiyo jana.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment