Mwanafunzi wa kidato cha 3 achomeka hadi kufa
Published on: May 20, 2017 08:26 (EAT)
Mwanafunzi wa kidato cha tatu ameaga dunia kwenye mkasa wa moto uliotokea jana usiku katika shule ya Bar-Kowino iliyoko Bondo kaunti ya Siaya.
Usimamizi wa shule hiyo unadai kuwa mwanafunzi huyo alikuwa na maumivu na kuamua kulala badala ya kujiunga na wenzake katika masomo ya jioni. Maskini bweni lilishika moto na mwanafunzi huyo akachomeka hadi kufa. Uchunguzi unaendelea kubaini chanzo cha moto huo.
Want to send us a story? Submit on Wananchi Reporting on the Citizen Digital App or Send an email to wananchi@royalmedia.co.ke or Send an SMS to 25170 or WhatsApp on 0743570000
Comments
No comments yet.
Leave a Comment