Naibu wa rais azuru Makueni na Kajiado
Naibu Rais William Ruto amemweleza mgombea mwenza wa kiti cha urais kwa tiketi ya Nasa Kalonzo Musyoka kuwa anapoteza wakati wake kwenye upinzani ambapo anafahamu vyema kuwa hana cha kuvuna. Ruto ambaye aliendeleza kampeni za Jubilee katika kaunti za Makueni na Kajiado amewataka wenyeji wa kaunti ya Kajiado kutobahatisha katika kinyang’anyiro cha Agosti . Huku haya yakijiri viongozi wa Nasa wameishtumu serikali kwa kushindwa kuthibiti mfumko wa bei za bidhaa. Kiongozi wa ODM Raila Odinga, akijibizana hadharani na mbunge wa Mumias Magharibi Benjamin Washiali anayepigia debe chama cha Jubilee huko Mumias.
Want to send us a story? Submit on Wananchi Reporting on the Citizen Digital App or Send an email to wananchi@royalmedia.co.ke or Send an SMS to 25170 or WhatsApp on 0743570000
Comments
No comments yet.
Leave a Comment