Nasa yazidi kujiimarisha Ukambani
Published on: September 08, 2017 08:05 (EAT)
Muungano wa Nasa umejizatiti kushikilia ngome zao ambapo wanawarai wafuasi wao kujitokeza kwa wingi katika marudio ya uchaguzi ili kuwapa Raila Odinga na Kalonzo Musyoka ushindi. Viongozi hao ambao walikuwa katika kaunti ya Machakos hii leo walitaja eneo hilo kama moja wapo ya maeneo ambapo kura zao za urais na ugavana ziliibiwa. Aidha wamewataka wafuasi wao kusimama imara na kutoshurutishwa na wale ambao wamehamia Jubilee baada ya kushindwa.
Want to send us a story? Submit on Wananchi Reporting on the Citizen Digital App or Send an email to wananchi@royalmedia.co.ke or Send an SMS to 25170 or WhatsApp on 0743570000
Comments
No comments yet.
Leave a Comment