Nkaissery, Omamo wawaonya wapinzani
Published on: June 23, 2017 08:13 (EAT)
Waziri wa ulinzi Racheal Omamo na mwenzake wa usalama wa ndani Jospeh Nkaisery wamesisitiza kuwa maafisa wa usalama wataendelea kutekeleza wajibu wao bila ya kuegemea upande wowote wa kisiasa, ama mapendeleo ya aina yoyote.
Wakihudhuria kufuzu kwa maafisa waliopokea mafunzo spesheli ya usalama wa kabla, wakati, na baada ya uchaguzi mkuu ujao, mawaziri hao wamewauliza maafisa wa usalama kupuuzilia mbali vitisho kutoka kwa wanasiasa.
Want to send us a story? Submit on Wananchi Reporting on the Citizen Digital App or Send an email to wananchi@royalmedia.co.ke or Send an SMS to 25170 or WhatsApp on 0743570000
Comments
No comments yet.
Leave a Comment