NOCK yapata kibarua kigumu kujibu maswali kuhusu bajeti ya RIO
Published on: September 14, 2016 09:16 (EAT)
Wanachama wawili wa kamati kuu ya Olimpiki watasafiri kuelekea Laussanne, Uswizi usiku wa leo kwa mkutano na kamati kuu ya Olimpiki duniani IOC. IOC imewaalika wawili hao pamoja na waziri wa michezo Hassan Wario. Wanachama wa kamati ya muda ya NOCK pia wamealikwa kwa mkutano huo baada ya waziri Wario kuvunja kamati kuu ya Olimpiki nchini wiki mbili zilizopita. Hayo yakijiri, NOCK ilikuwa na wakati mgumu hii leo walipofika mbele ya kamati maalum ya bunge kujibu maswali kuhuhu bajeti ya timu ya kenya.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment