ODM yatishia maandamano kupinga ufisadi
Published on: November 07, 2016 09:00 (EAT)
Mjadala kuhusu nani mhusika mkuu wa sakata ya mamilioni ya fedha za NYS umeendelea kwa siku ya tatu mfululizo leo ikionekana kuwa zamu ya upinzani kulivalia njuga suala hilo na kadhia nzima ya kashfa za ufisadi nchini. Wachambuzi nao wamejitosa katika suala hilo na kama anavyotupasha Salim Swaleh ni kwamba licha ya Naibu Rais kuondoka nchini na Waiguru kukaa kimya, moto waliouwasha unaendelea kuwaka kwa mpigo.
Want to send us a story? SMS to 25170 or WhatsApp 0743570000 or Submit on Citizen Digital or email wananchi@royalmedia.co.ke
Comments
No comments yet.
Leave a Comment